• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

KITETO YAZINDUA MNADA WA MBAAZI KUPITIA MFUMO WA KIDIGITALI WA TMX

Imetumwa : August 12th, 2024

Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia vyama vya Ushirika AMCOS na Chama Kikuu ACU, Agosti 11,2024,  imezindua mnada wa zao la mbaazi kupitia mfumo wa kidigitali wa TMX unaomuwezesha mkulima kuuza mazao yake  kupitia mtandao ambapo ataweza kuuza kwa bei ya juu na kunufaika ili kuepuka walanguzi wa zao hilo.


Akizungumza na wakulima hao wa mbaazi Wilayani humo, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Remidius Mwema, amesema kuwa serikali imejipanga kumuinua mkulima wa mbaazi na kuhakikisha mkulima anauza mazao yake kwa faida. Aidha Mhe. Mwema amekemea vitendo vya baadhi ya walanguzi kupotosha juu ya mnada kupitia mfumo wa kidigitali.


"Ni muhimu kuwa wakweli kwa sababu lengo ni kumsaidia mkulima yeyote, kuna watu ni wakulima wakubwa wapo humu ndani wanaleta, lakini kwenda wewe kumlangua mtu ukaja wewe kunufaika hapa, inakuwa hutendi haki" DC Mwema.



Aidha, Meneja wa Chama Cha Msingi Matui AMCOS, Ndg. Emmanuel Keyaa, ameipongeza serikali kwa kuleta mfumo huu kwa wakulima wa mbaazi na kuomba ifanye hivyo kwa mazao mengine ili wakulima wafaidike.


Kwa upande wake Afisa Mwandamizi Biashara TMX, Shani Mringo, amesema lengo kubwa la mnada huo ni kuwakutanisha wauzaji na wanunuzi wa bidhaa ndani na nje ya nchi ili kuweza kufanya biashara moja kwa moja kupitia mfumo wa kidigitali na muuzaji kulipwa kwa bei iliopo sokoni ndani ya masaa 48.


Wakizungumzia kufurahishwa na mfumo huo wa kidigitali wa kuuza zao hilo, baadhi ya wakulima na wauzaji hao wa mbaazi wameipongeza serikali kwa kuleta mfumo huo wenye tija kwa mazao yao.


Katika mnada huo wa kwanza katika msimu huu ambao umefanyika Agosti 11, 2024 katika kata ya Matui, jumla ya tani 116 za mbaazi zimeuzwa kwenye mnada huo kwa wanunuaji watatu tofauti kwa wastani wa bei ya TZS 2,127.78 kwa kila kilo.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa