• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

GHARAMA YA KUMUONA DAKTARI HOSPITALI YA WILAYA YAPUNGUZWA

Imetumwa : October 23rd, 2024

Baraza la Madiwani Wilaya Kiteto limeridhia mabadiliko ya gharama za kumuona daktari katika Hospitali ya Wilaya kutoka TZS 12,000 hadi TZS 5,000.

Mabadiliko hayo yamepitishwa kwenye kikao cha Robo ya Kwanza cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Oktoba 22,2024 katika Ukumbi wa Maktaba ya Wilaya.

Akitoa ufafanuzi kuhusu mabadiliko hayo, Mwenyekiti wa Halmashauri (W) Kiteto, Mhe. Abdallah Bundala amesema kwamba wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kiteto walikua wanatoa TZS 12,000 ikiwa ni ada ya kumuona daktari na bado walikua wanaendelea kulipia gharama za huduma nyingine kama vile vipimo na dawa.

Baada ya Baraza hilo kupitisha mabadiliko hayo, kuanzia Oktoba 22,2024 wagonjwa wanaoenda kupata matibabu katika Hospitali ya Wilaya Kiteto, watakua wanalipa TZS 5,000 ikiwa ni ada ya kumuona daktari ila wataendelea kulipia gharama nyingine kama vile vipimo na matibabu.

Mhe. Bundala aliendelea kueleza kua ada ya kumuona daktari katika zahanati na vituo vya afya itaendelea kubaki TZS 7,000.

“Tofauti ni kuwa wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya walikua wanalipa TZS 12,000 kumuona daktari na kulipia huduma nyingine kama vile vipimo na dawa wakati wagonjwa katika zahanati na vituo vya afya wanalipa 7,000 gharama hiyo inajumuisha kumuona daktari pamoja na huduma nyingine kama vipimo na dawa. Hivyo gharama kwenye zahanati na vituo vya afya kwasasa itaendelea kuwa hiyohiyo 7,000 na inajumuisha huduma ikiwemo kumuona daktari, vipimo na dawa” amefafanua Mhe. Bundala.

Mabadiliko hayo ya bei yanakuja baada ya maagizo ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, ambaye alifanya ziara wilayani hapa mapema mwezi huu na kuagiza viongozi wa wilaya kukaa na kuangalia namna ya kupunguza gharama hizo ili kumuwezesha mwananchi kupata huduma za afya hospitalini hapo kwa bei nafuu.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • AFYA NI MTAJI, TUJITOKEZE KWENDA KUPATA HUDUMA ZA KIBINGWA

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa