• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kilimo,umwagiliaji na ushirika

IDARA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

MUUNDO WA IDARA

Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ni Idara ambayo inasimamia na kutekeleza shughuli zote za kilimo cha mazao, usalama wa chakula na maendeleo ya Ushirika katika Wilaya.

Ofisi za Idara ya Klimo, Umwagiliaji na Ushirika pamoja na Idara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Wilaya Kiteto, zilizopo katika Mji mdogo wa Kibaya.

Idara hii inaundwa na sehemu (section) 10 ili kuwezesha utekelezaji wa shughuli zote za kila siku. Sehemu hizo ni Ushirika na Masoko, Huduma za Ugani,  Uzalishaji wa Mazao, Takwimu – Kilimo, Pembejeo za kilimo na Afya ya Mimea, Mipango na Matumizi bora ya Ardhi katika Kilimo, Kilimo cha Umwagiliaji, Kilimo cha Mboga mboga na Matunda,  Zana na mashine za Kilimo na  Lishe katika Kilimo.

IDADI YA WATUMISHI

Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika ina jumla ya Watumishi wa kudumu 63 kati yao Watumishi 16 ni Wanawake na 47 ni Wanaume kufikia mwezi Machi 2018.

Watumishi walioko kazini :

Wataalam wa Kilimo      59

Wataalam wa ushirika    03 (1 ni wa Tume ya Ushirika)

Katibu Muhtasi              00

Mhudumu                     01          

Upungufu wa Watumishi :

Idara ina upungufu wa Watumishi 39 kwa mchanganuo ufuatao

Wataalam wa Kilimo 36

Wataalam wa Ushirika  2

Katibu Muhutasi 1

MAJUKUMU YA MSINGI YA IDARA YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA

MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA USHIRIKA NA MASOKO

  • Kuhamasisha Jamii na kuongoza taratibu za uanzishwaji wa Vyama na Vikundi vya Ushirika Wilayani.
  • Kusimamia na kuratibu shughuli za Ushirika Wilayani, kuhakikisha kuwa zinatekelezwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za ushirika.
  • Kufanya ukaguzi wa Vyama vya Ushirika, ili kusimamia na kudhibiti mwenendo wa mapato na matumizi ya vyama.
  • Kufanikisha usajili wa Vyama vya Ushirika Wilayani kwa kushirikiana na Ofisi ya Mrajis wa Vyama vya Ushirika.
  • Kulea Vyama vya Ushirika Wilayani kwa kuhakikisha kuwa uendeshaji wake unazingatia taratibu, kanuni na sheria zinazoongoza ushirika Nchini.
  • Kutoa miongozo na mafunzo kwa wakati kwa Maafisa Ushirika wa Tarafa, Viongozi wa Vyama vya Ushirika na wanachama kuhusu Ushirika, Masoko na Ujasiriamali kwa minajili ya kuongeza ufanisi wa uendeshaji wa Taasisi hizi.
  • Kutoa ushauri wa Kitaalamu wa kufanikisha uendeshaji wenye tija wa Vyama vya Ushirika.
  • Kutoa ushauri, miongozo na msaada wa kitaalamu wa namna bora ya kufikia malengo ya msingi ya uanzishwaji wa vyama vya ushirika husika (yaani masoko, mitaji, nk.).
  • Kuratibu Ushiriki wa Sekta ya Umma na Binafsi katika uimarishaji wa shughuli za Ushirika pasipo kuathiri sheria, kanuni na taratibu za Ushirika.
  • Kuviongoza Vyama vya Ushirika katika utekelezaji wa majukumu yao ya Kikatiba, Kisheria na kikanuni.

2. MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA HUDUMA ZA UGANI

  • Kuongoza, kusimamia na kuratibu mahusiano ya kitaalamu baina ya Utafiti, Huduma za Ugani na Wakulima, ili kuhakikisha uwepo wa mawasiliano yenye tija ya Utaalamu wa kilimo.
  • Kuratibu shughuli za ugani Wilayani zinazotekelezwa kwa mbinu mbalimbali za mashamba darasa, mashamba ya mfano, mashamba ya majaribio, vikundi vya wakulima, maonesho, n.k.
  • Kupanga na kuratibu utolewaji wa mafunzo kwa Wataalamu wa Ugani na Wakulima Wilayani.
  • Kuratibu mtawanyiko wa maafisa ugani Wilayani kwa kuzingatia maeneo na uzalishaji wa mazao ya kilimo, ili kuongeza tija ya huduma ya ugani kwa kutumia raslimali watu iliyopo.
  • Kuongoza, kuratibu na kusimamia utaratibu wa utolewaji na utekelezwaji wa huduma za ugani Wilayani.
  • Kuratibu na kufuatilia shughuli za Wadau wa Kilimo Wilayani na shughuli wanazozifanya ili kuhakikisha kuwa wanayafikia malengo yao kwa manufaa ya wakulima na sekta nzima ya Kilimo.
  • Kuratibu, kuongoza na kuandaa maonesho ya kilimo na bidhaa zake katika ngazi mbalimbali.
  • Kumsaidia Mkuu wa Idara katika kuandaa na kusimamia utekelezaji wa Mpango wa Utekelezaji wa huduma za Ugani Wilayani.
  • Kuandaa machapisho na maandiko ya kilimo (kama vile Vipeperushi, Vijarida, Vijitabu na machapisho mengine) kwa ajili ya Wataalamu wa Ugani na hata Wakulima.
  • Kushirikiana na Wataalamu wengine katika kubaini na kutanzua changamoto za kilimo Wilayani.
  • Kuandaa taarifa ya Mwezi, Robo mwaka na mwaka ya huduma za ugani Wilayani.
  • Kuratibu shughuli za Vikundi na Majukwaa ya Kilimo Wilayani kwa ajili ya kuviwezesha kuyafikia malengo yao katika kuimarisha kilimo.
  • 3. MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA MBOGAMBOGA NA MATUNDA 
  • Kuratibu na kusimamia kilimo cha mbogamboga na matunda Wilayani
  • Kutoa mafunzo, ushauri na maelekezo ya kitaalamu kwa Maafisa ugani na Wakulima kuhusu kilimo cha mbogamboga na matunda.
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala kilimo cha mbogamboga na matunda.
  • Kuratibu usindikaji wa mazao ya mbogamboga na matunda kwa kutumia teknolojia mbalimbali
  • Kuandaa taarifa za kitaalamu kuhusiana na kilimo cha mbogamboga na matunda, pamoja na taarifa za kila mwezi, robo mwaka na mwaka.
  • Kutambua matunda na mbogamboga asilia zinazozalishwa na kutumika, pamoja nafursa za kuziendeleza na kuzihifadhi kwa ajili ya matumizi ya sasa na ya baadaye.

4. MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA CHAKULA NA LISHE KATIKA KILIMO 

  • Kuratibu na kusimamia shughuli za lishe-kilimo Wilayani, zilizojikita katika ubora wa mazao ya kilimo.
  • Kusimamia na kuratibu shughuli za usindikaji wa mazao ya kilimo ili kuona ubora wa bidhaa zinazosindikwa unazingatia kiwango cha lishe tarajiwa na kinaepuka uwezekano wa kuingizwa au kuzalishwa kwa sumu au kemikali zenye madhara kwa binadamu, mifugo na mazingira
  • Kuratibu shughuli za hifadhi salama ya mazao katika miundomsingi na teknolojia ya hifadhi ya mazao iliyopo, na kutoa ushauri wa Kitaalamu wa namna bora ya kuiboresha ili kuongeza tija ya hifadhi pasipo kuathiri ubora wa mazao yanayohifadhiwa.
  • Kutoa ushauri na mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani kuhusu usalama wa chakula, hifadhi salama ya mazao na lishe katika Kilimo.
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala ya chakula na lishe.
  • Kufanya tathmini ya hali ya chakula na lishe ili kuweza kushauri kuhusu hatua za kuchukuliwa kukabiliana nayo.
  • Kushiriki katika tafiti, na shughuli zinazohusiana na ubora wa chakula na lishe katika kilimo Wilayani.
  • Kuratibu mwenendo na maendeleo ya Viwanda vinavyosindika bidhaa za kilimo Wilayani.

5. MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA PEMBEJEO ZA KILIMO 

  • Kuratibu na kusimamia shughuli za usambazaji na upatikanaji wa pembejeo za kilimo Wilayani.
  • Kusimamia na kuratibu shughuli za Wasambaza Pembejeo za kilimo Wilayani ili kuona kuwa zinatekelezwa kwa kuzingatia ubora wa pembejeo hizo hadi zinapomfikia Mkulima.
  • Kukagua uwezo wa mbegu kuota ili kujiridhisha na ubora wa pembejeo hizo Wilayani kabla ya kuanza kwa msimu.
  • Kutoa ushauri na mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani kuhusu ubora wa pembejeo za kilimo na namna ya kutambua bidhaa hafifu na bandia sokoni.
  • Kufanya utafiti wa udongo na kiwango cha rutuba kilichopo kwa kushirikiana na Taasisi zilizopo Nchini.
  • Kuwasiliana na Taasisi zinazojishughulisha na pembejeo nchini ili kubaini mwenendo wa uzalishaji na bei ya bidhaa hizo, katika kuweka udhibiti wa bidhaa bandia na hafifu.
  • Kukagua na kusimamia ubora wa pembejeo za kilimo Wilayani kwa kushirikiana na Mamlaka husika.
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala ya uzalishaji, usambazaji, utoaji wa huduma za ugani na utafiti kuhusu pembejeo za kilimo na ufanisi wake.
  • Kufanya tathmini ya matumizi ya pembejeo ya kilimo na mchango wake katika kuboresha uzalishaji wa mazao katika msimu husika.
  • Kushiriki katika tafiti, na shughuli zinazohusiana na matumizi ya pembejeo za kilimo katika uzalishaji wa mazao Wilayani.
  • Kutafuta, kutambua na kuhifadhi pembejeo za asili kwa ajili ya matumizi ya baadaye katika kuinua uzalishaji wa mazao Nchini.
  • Kuandaa taarifa za kitaalamu kuhusu pembejeo za kilimo na matumizi yake salama katika uzalishaji wa mazao.
  • Kuratibu afya ya mimea na kushiriki katika udhibiti wa Visumbufu vya mazao, milipuko na majanga yaletwayo na Visumbufu hivyo kwa kushirikiana na Wadau husika.

6. MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA ZANA ZA KILIMO NA MITAMBO 

  • Kuratibu na kusimamia matumizi ya zana za kilimo Wilayani kwa kuzingatia kiwango na uwezo wa uhitaji wa teknolojia katika shughuli zote za kilimo kuanzia uandaaji mashamba hadi masoko.
  • Kutoa ushauri na maelekezo ya kitaalamu kwa Wakulima kuhusu mahitaji sahihi na ubora unaostahili wa zana za kilimo kwa ajili ya kukidhi mahitaji yao katika maeneo waliyopo.
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu kuhusu ubora wa zana za kilimo, mashine na mitambo, matumizi sahihi na matunzo yake.
  • Kutoa ushauri na mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani kuhusu zana za kilimo, mashine na mitambo.
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala ya zana za Kilimo, pamoja na matumizi yake.
  • Kufanya tathmini ya matumizi ya zana za kilimo, mashine na mitambo katika uzalishaji wa mazao na bidhaa zake Wilayani.
  • Kuandaa taarifa za kitaalamu kuhusiana na zana za kilimo, mashine na mitambo pamoja na matumizi yake.
  •  
  • 7. MAJUKUMU KATIKA SEHEMU YA MIPANGO NA MATUMIZI BORA YA ARDHI KATIKA KILIMO 
  • Kuratibu na kusimamia mipango na matumizi bora ya rasilimali ardhi katika shughuli za kilimo Wilayani.
  • Kutoa ushauri na maelekezo ya kitaalamu kwa Maafisa Ugani na Wakulima kuhusu matumizi yenye tija ya raslimali ardhi katika kufanikisha shughuli za kilimo kiuendelevu.
  • Kutambua uwepo wa uharibifu wa udongo na mazingira unaosababishwa na nguvu asilia au shughuli za kibinadamu na kupendekeza njia salama na zenye tija za kukabiliana nao.
  • Kutoa mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani kuhusu mbinu mbalimbali za kukabiliana na uharibifu wa udongo.
  • Kupima ubora wa udongo kwa ajili ya matumizi ya kilimo kwa kushirikiana na Taasisi zinazohusika Nchini
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala ya mipango na matumizi bora ya ardhi katika kilimo.
  • Kuandaa taarifa za kitaalamu kuhusiana na mipango na matumizi bora ya ardhi katika kilimo.
  • Kufanya ufuatiliaji wa mwenendo wa hali ya hewa Wilayani kwa kushirikiana na Taasisi husika, na kusambaza taarifa hizo kwa Wadau wote wahusika.
  • Kushiriki katika timu ya wilaya ya usimamizi shirikishi wa mipango ya matumizi bora ya ardhi

8. MAJUKUMU YA SEHEMU YA UZALISHAJI WA MAZAO 

  • Kufuatilia mwenendo wa uzalishaji mazao ya chakula na biashara mashambani.
  • Kufuatilia afya ya mimea na udhibiti wa Visumbufu na magonjwa ya mazao pindi yajitokezapo mashambani na katika hifadhi ya mazao.
  • Kutoa mafunzo, ushauri na maelekezo ya kitaalamu kwa Maafisa ugani na Wakulima kuhusu uzalishaji wenye tija wa mazao na udhibiti wa Visumbufu vya mazao na magonjwa.
  • Kufanya majaribio ya teknolojia mbalimbali za uzalishaji wa mazao Wilayani.
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala ya uzalishaji wa mazao na teknolojia zake.
  • Kufanya tathmini ya hali ya mazao na afya ya mimea mashambani.
  • Kuandaa taarifa za kitaalamu kuhusiana na hali ya mazao, uzalishaji wake na afya ya mimea.
  • Kuandaa Mpango wa muda mfupi na mrefu wa maendeleo ya kilimo na udhibiti wa magonjwa na Visumbufu vya mazao Wilayani.
  • Kufanya ufuatiliaji na kuratibu mwenendo wa hali ya hewa na viashiria vya kujitokeza kwa majanga yanayohusiana na kilimo, na kufanya mawasiliano kwa wakati na Mamlaka husika na Wadau.
  • Kuatmbua na kuhifadhi mazao asilia na mbegu asilia za mazao kwa ajili ya kuhifadhi vinasaba kwa ajili ya matumizi ya sasa na baadaye
  • Kutambua na kubaini aina ya pembejeo bora za kilimo zilizopo sokoni zinazoendana na tabianchi na mazingira ya Wilaya hii.

9. MAJUKUMU YA SEHEMU YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI 

  • Kuratibu na kusimamia shughuli za kilimo cha umwagiliaji zinazofanyika katika Skimu na kwa Mkulima mmojammoja Wilayani.
  • Kutoa ushauri na maelekezo ya kitaalamu kwa Maafisa Ugani na Wakulima wamwagiliaji kuhusu teknolojia za kilimo cha umwagiliaji na matumizi yenye tija ya raslimali maji katika kilimo cha umwagiliaji.
  • Kusimamia matumizi yenye tija na ufanisi tarajiwa ya miundombinu ya umwagiliaji katika Skimu za kilimo cha umwagiliaji Wilayani.
  • Kutoa mafunzo kwa Wakulima na Maafisa Ugani kuhusu kilimo cha umwagiliaji na teknolojia zake.
  • Kushirikiana na Wadau wa Kilimo Wilayani wanaojishughulisha na masuala ya kilimo cha uwagiliaji.
  • Kufanya mawasiliano na Taasisi inayojishughulisha na Kilimo cha Umwagiliaji Nchini ili kuimarisha mfumo wa mawasiliano kwa ajili ya maendeleo ya kilimo hicho Wilayani.
  • Kuandaa taarifa za kitaalamu kuhusiana nakilimo cha umwagiliaji Wilayani.
  • Kuandaa Mpango wa Maendeleo ya Kilimo cha Umwagiliaji Wilayani

10. MAJUKUMU YA SEHEMU YA TAKWIMU KILIMO 

  • Kuratibu uandaaji, ukusanyaji, usanifu, uhifadhi wa takwimu kilimo na kuziwasilisha katika Mamlaka husika na kwa wadau kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za takwimu Nchini.
  • Kushiriki kuandaa, kusimamia na kutathmini utekelezwaji wa Miradi ya maendeleo ya kilimo inayotekelezwa Wilayani na Serikali pamoja na Wadau wengine wa kilimo.
  • Kuandaa na kusimamia bajeti ya Idara na Mpango wa Wilaya wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (DADPs) kwa kushirikiana na Wataalamu wote wa Idara na kuiwasilisha katika Ofisi husika kwa wakati.
  • Kutoa ushauri, maelekezo na mafunzo kwa Maafisa Ugani kuhusu takwimu kilimo, umuhimu wake na mbinu bora za uandaaji na ukusanyaji wake.
  • Kuhakiki ubora wa takwimu kilimo zilizokusanywa na Maafisa Ugani, pamoja na Wadau wengine na kuzihariri pamoja na kuzichambua na kuzihifadhi kwa ajili ya matumizi ya Idara na wadau wengine.
  • Kuandaa taarifa za mwezi, Robo mwaka na Mwaka za kilimo na kuziwasilisha katika Ofisi husika kwa wakati.

WADAU WA MAENDELEO YA KILIMO, UMWAGILIAJI NA USHIRIKA WILAYANI:

Serikali katika Wilaya ya Kiteto, inafanya kazi katika kuleta maendeleo ya Kilimo ikiwa sambamba na Taasisi za Kiserikali, Sekta Binafsi, Mashirika ya Kimataifa, Taasisi za Kidini, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, na Taasisi nyingine. Wadau hawa hushiriki katika kutoa huduma za ugani kwa kusaidia uenezaji wa teknolojia mpya au zenye tija Wilayani, Kuandaa na kusaidia uanzishaji au ujenzi wa miundombinu ya Kilimo na kufanya utafiti wa teknolojia mbalimbali ndani ya Wilaya. Wadau hawa ni pamoja na:

  • Mashirika ya Kimataifa: kama vile FAO, CIMMYT, IITA, ICRAF, USAID, AVRDC (The World Vegetable Centre), WFP
  • Taasisi za Utafiti wa kilimo za Kiserikali: Kituo cha Utafiti-Kilimo Hombolo, Kituo cha Utafiti-Kilimo Selian, Kituo cha Utafiti-Kilimo Horti-Tengeru, Kituo cha Utafiti-Kilimo Ilonga.
  • Taasisi za Kidini: Kama vile Norwegian Church Aid (Kwa kushirikiana na Dayosisi ya Kanisa Anglican, Morogoro), n.k.
  • Asasi zisizo za Kiserikali: kama vile KINNAPA, FIPS, CORDS, MVIWATA, CFU/TAP, RUDI Farm Africa.
  • Sekta Binafsi: kama vile Makampuni ya pembejeo za kilimo ya SUBA Agro, Kibo Seed Co. Ltd, Zamseed (T) Ltd, Meru Agro-Consultant Ltd, Kiteto AgroBusiness Ltd, SEEDCO Ltd, nk.
  • Taasisi za kifedha: kama vile Benki ya Kilimo Tanzania (TADB), NMB nk

SHUGHULI ZA KILIMO:

Wilaya ina eneo lenye ukubwa wa Hekta 382,000 zinazofaa kwa kilimo, na kati ya hizo, takriban hekta 208,000, ndizo zinazotumika katika shughuli za kilimo, Mazao ya aina mbili hulimwa hapa Wilayani ambayo ni mazao ya chakula na mazao ya biashara. Mazao makuu ya chakula yanayolimwa ni Mahindi, Mtama na Maharage. Mazao makuu ya biashara yanayolimwa ni Alizeti, Mbaazi na Ufuta. Kilimo katika Wilaya hii huendeshwa kwa takriban asilimia 99.9, kwa kutegemea mvua, hasa kutokana na uwepo wa kiwango kidogo cha vyanzo vya maji vya kudumu.

Kilimo cha mahindi kinachoendeshwa kimseto na zao la mbaazi, ni mojawapo ya mbinu za kilimo zinazofanywa na wakulima wengi kwa lengo la kuongeza tija kimapato katika eneo linalotumika katika uzalishaji.

Kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2012, asilimia 58 ya Wakazi wote wa Wilaya ya Kiteto hujishughulisha na kilimo, kama shughuli yao ya msingi kwa ajili ya kuzalisha chakula na kujiongezea kipato.


           Alizeti zao la mafuta ambalo linategemewa kibiashara na wakulima wengi wa Wilaya ya Kiteto

Uwele, mojawapo ya zao la chakula linalozalishwa Wilayani Kiteto, lenye uwezo wa kufanya vizuri kiuzalishaji katika eneo la nyanda kame kama Wilaya hii.
Kilimo cha mtama, mojawapo ya mazao yanayostahimili ukame na kuzalishwa kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya chakula na Wakulima wa Kiteto

Kiteto inapatikana katika eneo ambalo linajumuisha hali ya hewa na tabianchi zinazotofautiana katika baadhi ya maeneo, hivyo kutoa fursa ya kuendesha uzalishaji wa mazao anuwai (Crop Diversity) ndani ya Wilaya. Lakini, sehemu kubwa imo katika eneo lenye nyanda kame, hivyo matumizi ya teknolojia na mbinu mbalimbali za kukabiliana na hali hiyo, pasipo kuathiri uzalishaji hutumika katika uzalishaji. Hii ni pamoja na matumizi ya mbinu na teknolojia za kilimo hifadhi na jembe-makucha la trekta au tindo/Ripa ya trekta (Ripper) kwa ajili ya kutindua udongo na kuvuna maji ya mvua mashambani.

Mbinu ya kutindua udongo kwa kutumia jembe–tindo/ripa linalokokotwa na trekta, kama mojawapo ya teknolojia inayotumika katika kuvunja jasi kwenye udongo na kuvuna maji ya mvua kupitia mbinu za kilimo hifadhi.

Uandaaji wa mashamba kwa ajili ya kufanikisha kilimo cha mazao katika Wilaya hii hutekelezwa kwa kutumia zana bora za kilimo, ambapo takriban 84% hutumia matrekta makubwa, matrekta madogo (Powertiller), pamoja na zana zinazokokotwa na Wanyamakazi. Hali hii huongeza tija katika uandaaji wa mashamba, na kupunguza ugumu wa kazi ya uandaaji.

Mkulima akiandaa shamba lake kwa kutumia trekta, ikiwa ndio njia kuu inayofanywa na Wakulima wa Kiteto katika kufanikisha shughuli zao za uzalishaji mashambani.

 

SHUGHULI ZA UMWAGILIAJI

Wilaya ya Kiteto, inaendesha kilimo cha umwagiliaji, hasa cha mazao ya mbogamboga katika maeneo mbalimbali kwa kutumia vyanzo vya maji vilivyopo. Wilaya ina takriban ekari 37.5 zinazotumika katika kuendeshea kilimo hiki. Mazao ya mbogamboga yanayozalishwa ni pamoja na Mboga za Majani, Nyanya, Vitunguu, Ngogwe/Nyanya Chungu, Bamia,n.k. Maeneo yote humwagiliwa kwa kutumia teknolojia ya umwagiliaji wa moja kwa moja (Surface Irrigation), ila kuna ekari 5 zilizoendelezwa kwa teknolojia ya matone (Drip Irrigation) katika kijiji cha Olgira

        Kilimo cha umwagiliaji kwa kutumia tekinolojia ya matone katika Skimu ya Umwagiliaji Olgira

Changamoto kubwa ya kilimo cha umwagiliaji katika Wilaya hii ni ukosefu wa mito inayotiririsha maji mwaka mzima na hivyo kufanya kilimo hiki kuwa cha kubahatisha.

Maendeleo ya Kilimo katika sekta hii hutekelezwa kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa mazao yenye virutubisho vingi (kama vile mbogamboga na matunda) ndani ya Wilaya ili kupambana na Athari zinazoikabili jamii kutokana na lishe, hasa utapiamlo. Jitihada hizi hulenga katika kutoa mbinu ya kukabiliana na tatizo hilo kwa kuwapatia chakula kinachoundwa na mlo kamili Wanajamii wote ili kulikabili tatizo la uwepo wa utapiamlo kwa takriban 0.6% ya Watoto wadogo wenye umri wa chini ya miaka mitano, ndani ya Wilaya, hali inayotishia afya zao za kimwili na ubongo. Vilevile, Kilimo hiki ni chenye uhakika, hivyo kuchangia katika kuimarisha hali ya usalama wa chakula ngazi ya Kaya na kipato; hivyo kufanikisha vita dhidi ya Maadui Ujinga, Maradhi na Umasikini.

MAFANIKIO YA SEKTA YA KILIMO

  1. Kufanikisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya kilimo kama vile uboreshaji wa miundombinu ya umwagiliaji kwa njia ya matone katika skimu 1 iliyopo katika Kijiji cha Olgira, ujenzi wa maghala 3 ya kuhifadhia mazao katika vijiji vya Olgira, Magungu na Orkine, ujenzi wa vituo 3 vya wakulima katika Kata za Njoro, Engusero na Kibaya na kuwezesha vikundi 85 vya kilimo kupata na kutumia tekinolojia mbali mbali za kilimo.
  2. Kufanikisha utolewaji wa huduma za ugani kwa wakulima kwa kushirikiana na Sekta binafsi na wadau mbalimbali wa kilimo katika vijiji vyote vya wilaya.
  3. Ujenzi wa soko la mazao katika kijiji cha Sunya unaendelea ili kuwezesha wakulima wa kata ya Sunya kupata soko bora la mazao yao.

SHUGHULI ZA USHIRIKA:

Moja ya majukumu ya Idara ni kusimamia na kuendeleza shughuli za Ushirika, Wilaya ina Vyama vya Ushirika 41 vinavyojishughulisha na kuwaunganisha Wakulima/Wafugaji katika makundi yenye malengo ya kimaendeleo katika kuinua hali zao za kiuzalishaji, kujipatia mitaji ya kuwekeza katika shughuli zao za kiuchumi na masoko ya mazao yao. Kati ya hivyo, vipo Vyama vya ushirika vya masoko ya Kilimo (AMCOS) 16, vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) 23 na Ushirika wa Viwanda (Industrial Cooperatives) 2 na chama cha Ushirika wa Maziwa (DairyCooperative Society) 1.

 

Kiwanda kidogo cha Ushirika wa Wazalishaji wa maziwa Kibaya (KDC), kilichopo katika Mji mdogo wa Kibaya
 

TAKWIMU ZA VYAMA VYA USHIRIKA HADI APRIL, 2018

AINA YA CHAMA

IDADI YA WANACHAMA

ME
KE
VIKUNDI
TAASISI
JUMLA
AMCOS
817
495
0
0
1312
SACCOS
895
670
39
0
1604
LIVESTOCK  COOPERATIVE
22
39
0
0
61
DAIRY COOPERATIVE
12
23
0
0
35
INDUSTRIAL COOPERATIVE
2
28
0
0
30
JUMLA
1748
1255
39
0
3042

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • Tangazo kwa wanainchi wa Kiteto nafasi za ajira toka jeshi la uhamiaji January 02, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE KITENGO CHA AFYA KINGA KWA KIPINDI CHA ROBO YA KWANZA JULAI - SEPTEMBA 2022

    October 21, 2022
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA LISHE KIPINDI CHA ROBO YA PILI (OCTOBA-DISEMBA 2021)

    January 24, 2022
  • Maafisa wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto wakiwa wanapitia rejea ya mafunzo ya PLANREP iliyoboreshwa

    December 22, 2021
  • Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mh.Mbaraka Al Haji Batenga akizungumza kwenye kikao cha maendeleo ya Wilaya (DCC)

    December 16, 2021
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa